Timu inayocheza katika ligi kuu ya Premier ya Blackburn Rovers, sasa imenunuliwa na familia ya Rao kutoka India, kwa pauni milioni 43.
Taasisi iliyoanzishwa na aliyekuwa mmiliki wa klabu, Jack Walker, imeuza hisa zake, asilimia 99.9, kwa kampuni ya Vencky London Ltd.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Paul Egerton-Vernon amesema: "Tumefurahi sana kuikabidhi familia ya Rao timu ya Rovers".
"Tumefurahishwa na namna walivyoitamani timu, na mipango na mawazo yao kuhusiana na uwekezaji zaidi, na pia mapenzi yao ya kuendelea kuendeleza kumbukumbu za Jack Walker".