Vurugu zimetokea katika makao makuu ya tume ya uchaguzi nchini Ivory Coast, baada ya wafuasi wa Rais Laurent Gbabgo kupinga kutangazwa kwa matokeo ya duru ya pili ya uchaguzi.
Mfuasi sugu wa Rais Gbabgo ambaye pia anahudumu kwenye tume ya uchaguzi, alizua utata pale alipochana karatasi iliokuwa na matokeo ya awali, akidai kuwa hayakuwa sahihi.