"Sidhani kama kuna timu nyingine zaidi yetu sisi, Chelsea au Arsenal", amesema Ferguson, ambaye timu yake ipo kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi mbili, huku ikiwa na michezo miwili viporo.
United huenda ikaongeza tofauti ya pointi, watakapocheza na Sunderland siku ya Jumapili iwapo watashinda. Arsenal iliyo katika nafasi ya pili itapambana na Chelsea iliyo nafasi ya nne, siku ya Jumatatu.
Ferguson ameongeza kuwa anahisi Manchester City na Tottenham zitashindwa kuendelea kupambana kuwania ubingwa.