Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Uingereza, Theresa May, anasema, anazingatia kama anafaa kumpiga marufuku kasisi mmoja wa Marekani, kuingia Uingereza au la.
Kasisi Terry Jones, alizusha tafrani ya kimataifa mapema mwaka huu, alipotangaza mpango wa kuchoma moto Koran, wakati wa kukumbuka mashambulio ya tarehe 11 Septemba.Kasisi Terry Jones, alisema kuwa anapanga kuzuru Uingereza, kuitikia mwaliko wa chama chenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia, English Defence League.

Wanaharakati wamesema, Kasisi Terry Jones akiingia nchini Uingereza, kunaweza kuzuka hisia dhidi ya WaIslamu.