Rais Jakaya Kikwete, amesema serikali itahakikisha matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea katika medani ya kisiasa jijini Arusha Jumatano wiki hii, hayatokei tena.
Alitoa kauli hiyo alipokutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini, katika hafla fupi ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2011, iliyofanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam jana.
Rais Kikwete alisema mwaka uliopita (2010), ulikuwa wa uchaguzi, ambao ulikabiliwa na changamoto nyingi.
Alisema anashukuru uchaguzi huo ulifanyika salama na kudhihirisha kwamba, demokrasia imekua nchini. Hata hivyo, alisema kuna matukio katika medani ya kisiasa yaliyolikumba jiji la Arusha hivi karibuni. “Tunatarajia matukio hayo yatakuwa ni ya mwisho kutokea,” alisema Rais Kikwete bila kutoa ufafanuzi.