Kampuni inayomiliki masuala ya umeme nchini Singapore imetangaza kuongeza bei ya umeme kuanzia tarehe 1 April mwaka huu.Kampuni hiyo ya SP imetangza kuwa wananchi wenye nyumba kuanzia vyumba vinne watalipa kiasi cha dola 4.85 zaidi kulingana na matumizi ya umeme huo.Ongezeko hilo la bei linatokana na kuongezeka kwa bei ya Petrol miezi mitatu iliyopita nchini humo.