Kuna taarifa zisizothibitishwa kwamba waziri wa ujenzi John Magufuli amejiuzulu wadhifa huo.Taarifa za kuaminika toka serikalini zimepasha kuwa waziri huyo amemuandikia barua Rais Jakaya Kikwete, akimtaarifu uamuzi wake wa kujiuzulu baada ya kufadhaishwa na hatua ya Waziri huyo, Mizengo Pinda kumuingilia katika utekelezaji wa majukumu ya wizara yake.

Vyanzo vimefafanua kuwa uamuzi huo umesababishwa zaidi na matukio ya hivi karibuni ya Pinda kukosoa hadharani kazi ya bomoa bomoa kwenye hifadhi ya barabara lililokuwa likitekelezwa na waziri huyo na kuagiza lisitishwe hadi hapo itakapo amuliwa vinginevyo na Baraza la Mawaziri.
JE NI KWELI?