Maafisa polisi wanne wameshtakiwa kwa kosa la mauaji baada ya kudaiwa kusababisha vifo vya watu wawili waliokuwa wakitazama mechi ya mpira baina ya timu za Chelsea na Manchester kwenye baa.
Polisi walisema baa hiyo ilikuwa iko wazi kinyume na sheria ikionyesha mechi ya ligi kuu ya soka ya England.

Wateja walikataa kuondoka kwenye baa hiyo na polisi walirusha mabomu ya kutoa machozi katika mji wa Mazabuka kusini mwa nchi hiyo.
Polisi walisema, hali hiyo ilisababisha watu kukurupuka ambapo mwanammke mmoja mwenye umri wa miaka 21 na mwanamme wa miaka 23 walifariki dunia.