Vodacom Miss Tanzania 2011, Salha Izrael (katikati) akiwa na baadhi ya warembo walioshiriki shindano la Miss Tanzania 2011 waliofika kumpokea katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana akitokea jijini London Uingereza alikoshiriki shindano la urembo la Dunia Novemba 6,2011. Warembo hao toka kushoto ni Jenifa Kakolaki, Alexia Willam,Hussna Maulid na Hamisa Hussein.