Kufuatia kunyesha kwa mvua nyingi hapa nchini, jiji la Mwanza leo limekumbwa na mafuriko yaliyosababisha hasara kubwa kwa wananchi wa jiji hilo. Kiwanja cha ndege jijini hapo kimefungwa na baadhi ya shughuli za ujenzi wa taifa zimesimama kutokana na mvua hizo kali. Kwa sasa wananchi wanajaribu kuokoa baadhi ya mali zao katika maeneo ambayo mafuriko hayo yameathiri zaidi.(Mabadiliko)