Mtangazaji wa siku nyingi na mwaasisi wa Shirika la Utangazaji la Tanganyika Broardcasting Cooparation (TBC) enzi hizo, na Radio Tanzania Dar es salaam (RTD) Mzee David Wakati amefariki dunia usiku wa kumakia leo. Habari zaidi na mipango ya mazishi tutaendelea kuwajulisha kwa yale yatakayojiri kuhusiana na msiba huo mkubwa kwa wanataaluma ya habari. Mzee David Wakati alikuwa ni mtangazaji mahiri na aliyeitangaza vyema Tanzania katika masuala ya habari kimataifa hasa alipokuwa akifanya kazi katika Idhaa ya Kikwashili ya Sauti ya Ujerumani jijini Born Ujerumani. Mungu aiweke roho ya marehemu David Wakati mahali pema peponi AMEN