Na.Datus Boniface
Mufti wa Tanzania, Issa Shaban Simba (pichani), ameitisha kikao cha dharula cha Baraza la Mauramaa kujadili juu ya hatua za kuzichukua kutokana na kutolewa kwa filamu inayodaiwa kukashimu dini ya Kiislam, huku akilaani filamu hiyo.
Aidha Mufti amewataka waumini dini hiyo kuwa watulivu wakati wakijiandaa kujadili suala hilo.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Bakwata ilisema, kikao hicho ndicho kitaamua la kufanya juu ya filamu husika.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mufti Shaban Simba amelaani kitendo cha kurushwa kwa filamu hiyo.