Stori: Maria Halimoja
Mkali wa sinema za Kibongo, Aunty Ezekiel amesema anatamani iwe leo au kesho apate mtoto kwani umri wake unaruhusu.Akipiga stori
mbili-tatu na paparazi wetu, Aunty alisema kuwa anatamani kuwa mama si kwa kufuata mkumbo bali anataka kuwa mama kwani sasa ni muda muafaka kwake.“Natamani kwelikweli na mimi siku moja niwe mama wa mtoto sema tu sijabahatika kupata ila naendelea kumuomba Mungu ili ndoto zangu ziweze kutimia,” alisema Aunty Ezekiel