Mfalme  wa muziki wa reggae barani Afrika Jhikoman alifanikiwa kufunika kwa kishindo kikubwa katika maonyesho ya 5th International African festival Tubingen,  siku ya jumapili 20 julai 2014 mjini Tubingen,Ujerumani.
Katika maonyesho hayo mwanamuziki Jhikoman kwa sasa ndiye nyota inayong'aa kutoka Afrika katika muziki wa reggae aliuthiirishia ulimwengu kuwa Tanzania ni moto wa kuotea mbali kimuziki ,akishagiliwa na umati wa maelefu ya washabiki waliofika katika maonyesho Jhikoman anatajwa ndie mfalme na nyota mpya ya muziki wa reggae kutoka Afrika,Jhikoman mwenye maskani yake Bagamoyo mkoani Pwani,Tanzania amepata bahati ya kukubalika na kupata mkataba na kutumbuiza katika maonyesho mengi barani ulaya.
(picha kwa niaba ya Afrika Festival Tubingen)