10514673_338168816341103_5043683657096333091_n
Bendi Mahiri na Machachari Jijini Dar Skylight Band wametoa wimbo wao wa Tano ikiwa ni muendelezo wa kutoa nyimbo tofauti tofauti kupitia Studio yao ya kisasa ya Skylight Production.
Akiongea na Mtandao huu Meneja wa Band hiyo Aneth Kushaba AK47 amesema wimbo huo unaitwa “Pasua Twende” ambo umetungwa na Mkurugenzi Mkuu wa bendi hiyo Dk. Sebastian Ndege akishirikiana na wanamuziki wa Bendi hiyo.
Aneth akaongezea kwamba wimbo huo ni wa tano kutolewa katika mtiririko wa nyimbo zao zilizokwisha kutoka na imetengenezwa ndani ya studio yao ya Skylight Production chini ya Produzya Joobanjo.
Isikilize hapa chini na Ijumaa hii utapa fursa ya kusikiliza ikipigwa LIVE ndani ya kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.