Shambulio dhidi ya makao makuu ya idara ya usalama ya Somalia mjini Mogadishu limeuwa watu 10.
Wakuu walisema saba kati ya hao ni wapiganaji wa al-Shabaab ambao waliingiza kwa nguvu gari lilojaa mabomu katika uwa wa jengo hilo ambalo lina ulinzi mkali.
Tena washambuliaji walijaribu kuingia ndani ya jengo.
Al-Shabaab ilisema ilifanikiwa kuwaachilia huru wafungwa wengi katika makao makuu hayo, ambayo yana gereza chini kwenye handaki na pahala pa kuhoji wafungwa.