Rais wa Urus Vladimir Putin.
Vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi vitaanza rasmi kutumika leo.
Hata hivyo, vitaondolewa vyote au baadhi yake tu mwezi ujao iwapo kutakuwa na maendeleo katika utekelezaji wa mpango wa amani wa Mashariki mwa Ukraine.
Uamuzi wa kutekeleza vikwazo hivi ulifikiwa jana baada ya mkutano wa pamoja kati ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron na viongozi wengine mashuhuri wa EU.
Mchakato huu ulicheleweshwa kwa siku kadhaa kwa hofu ya baadhi ya nchi kwamba vikwazo zaidi vitaharibu matarajio ya kusitishwa mapigano.
Vikwazo hivi vipya vinayalenga makampuni ya mafuta ya Urusi, sekta za fedha na ulinzi.
Pia wameongeza majina mengine 24 katika orodha ya maafisa wa Urusi na viongozi wa waasi nchini Ukraine ambao wanakabiliwa na kunyimwa visa na kuzuia mali zao.