Wadau mbalimbali wakiwasili kwenye hotel ya Millennium Durham tayari kwenye DICOTA 2014 utaonza rasmi Ijumaa Oct 3, 2014 kwenye mji wa Durham jimbo la North Carolina mkutano utamalizika siku ya Jumapili Oct 5, 2014 kwenye picha kushoto ni mpiga picha za kiwango na maarufu kutoka DMV Bi Iska Jojo na makamu wa rais DMV Bi, Harriet Shangarai wakielekea vyumbani baada ya kuwasili kwenye hotel ya Millennium muda si mrefu na kukutana na ukodak wa Vijimambo ambao utakuwepo kwenye mkutano huo kuwakilisha.
 Maafisa wa DICOTA wakihakiki usajili wa wadau waliofika mapema leo siku ya Alhamisi Oct 2, 2014 tayari kwa DICOTA 2014 Convetion.
 Wadau wakifuatilia usajili wao kuhakikisha kila kitu kipo sawa wadau wawili kushoto ni Suleiman Zanangwa na Focus wawakilishi wa Tanzania Ports Authority
Msanii wa vichekesho kutoka kundi la Zecomedy Masanja mkandamizaji akicheza na simu yake kutupia mawili matatu kwenye mitandao ya kijamii akiwa nae tayari kuwakilisha kwa mara ya kwanza katika historia ya DICOTA ndani ya Durham, North Carolina.


Wawakilishi toka Global Land Solutions toka Tanzania wakipata picha ya kumbukumbu kama walivyokutwa na kamera ya Vijimambo kwa picha zaidi bofya HAPA