Meja jenerali wa jeshi la Marekani bwana Greene
Rais wa Marekani Barack Obama amethibitisha wito wa kulitumia jeshi la nchi hiyo na wale wa akiba iwapo watahitajika kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola Afrika magharibi.
Rais Obama amesema wanajeshi hao wataongeza nguvu ya jeshi katika kutoa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo.
Kundi la kwanza la wanajeshi hao linatarajiwa kupelekwa kusaidia ujenzi wa vituo 17 vya kutolea tiba ya ugonjwa huo, katikati mwa Liberia, moja ya nchi iliyoathiriwa vibaya na ugonjwa huo.

Maafisa wa kikosi cha ulinzi wameelezea agizo hilo la Raisi Obama kama agizo la muhumu ili kuongeza kasi ya kutekeleza mipango ya kwenda kuisaidia mapambano ya ugonjwa huo
na itamfanya rais kutuma majeshi mengine zaidi iwapo watahitajika.
Marekani imeahidi kupeleka askari wake wapatao elfu nne huko Africa Magharibi kusaidia mapambano ya kuzuia na kuumaliza kabisa ueneaji wa ugonjwa wa Ebola.
Rais Obama amesema hajapinga wazo la kutekeleza katazo la kuziuia watu wanaoingia nchini Marekani kutoka nchi zilizo athiriwa na ugonjwa huo,na hadhani kama wazo hilo litafanikiwa.
Ameyasema hayo mwishoni mwa mkutano aloufanya katika ikulu ya Marekani na maafisa wa shirikisho juu ya ushiriki wa nchi ya Marekani katika mapambano na ugonjwa huo.
Raisi Obama amesema anaamini hatua za uchunguzi wa ugonjwa huo ni hatua nzuri.
Sina sababu za kifolosofia ya kupinga katazo la safari, kama hiyo ndiyo itakuwa ndiyo njia bora ya kuwaweka raia wa Marekani salama.tatizo ni kwamba je haya ndiyo majadiliano yangu niliyoyafanya a na wataalamu walioko kwenye maeneo ya tukio yaliyoathiriwa na ugonjwa huo ni kwamba katazo la safari halina nguvu kama hatua tulizochukua hivi karibuni kupambana na ugojwa huo.
Obama pia aesema yupo wazi kumteua atakayesimamia janga la Ebola
Mpaka hatua hii kila mtu binafsi amefanya kazi nzuri yenye kutukuka ,kazi ambayo ni ngumu kupambana na majimaji ya ugonjwa huu. Hii inatufanya tuwe kama mtu mmoja ,kwa sehemu baada ya janga hili tunaweza kusonga mbele kama kawaida.
Naye mkuu wa kitengo cha maendeleo ya kimataifa wa Marekani ameahidi kuongeza dola milioni mia moja na arobaini na mbili ili kusaidia mapambano ya ugonjwa wa Ebola huko Guinea.
Bwana Rajiv Shah aliyeko nchini Guinea kwenye ziara ya kujionea hali halisi ya athari zilizoletwa na ugonjwa huo Africa Magharibi, na kusema kwamba anafikiri msaada huo utarejesha matumaini ya watu waishio nchini humo.
Natangaza ongezeko la dola milioni moja na eflfu arobaini na mbili ili kuendeleza mapambano nchini Guinea katika ugonjwa wa Ebola,kwa vitengo vinavyojihusisha na ugonjwa huu,ili kuongeza ufanisi katika idara ya afya na wafanyakazi wake na kuongeza nguvu katika elimu juu ya ugonjwa huu.