Stori: Imelda Mtema
STAA wa filamu mwenye makeke mengi, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kwa mtazamo wake anaona Bongo Movies imebuma hivyo ameamua kukomaa na shule ili awe na kitu kingine tofauti na sanaa.Akizungumza na mwanahabari wetu, Lulu alisema kuwa kwa sasa yuko Chuo cha Uhazili Magogoni, Posta jijini Dar akichukua ‘course’ ya Utawala wa Umma (Public Administration) kwa ajili ya kupata ujuzi mwingine kichwani.
“Mwe-nzangu naona Bongo Movies kunaelekea kubaya, bora hata nikomae na shule angalau hata niwe na kitu kingine kichwani nipate mbadala wa sanaa,” alisema Lulu.