Baada ya wiki iliyopita kuwaletea mabinti warembo wa marais wa nchi kadhaa za Afrika wanaosifika kwa uzuri, wiki hii tunawaletea wake wa marais wa nchi hizo ‘wanaokimbiza’ kwa uzuri, uvaaji nk.Ana Paula Dos Santos 
alizaliwa1964, ni mke wa Rais wa Angola, Jose Eduardo Dos Santos, Paula ni mwanamitindo wa zamani, anasifika kwa uzuri na kujua kuvaa.Mama Salma Kikwete
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alizaliwa 1963, anatajwa kuwa katika orodha ya wake wazuri wa marais wa Afrika, anasifika kwa mavazi yake ya kitenge.Margaret Wanjiku Kenyatta
Ni mke wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, anatajwa kuwa na tabasamu zuri ingawa nywele zake zenye rangi ya kijivu ni kivutio kikubwa. Kazaliwa Mwaka 1963.Mialy Razakandisa Rajoelina 
Ni miongoni mwa wake vijana wa marais katika Bara la Afrika na anatajwa kuwa na ngozi nzuri na urembo wa asili, ni mke wa Rais Andry Rajoelina wa  Madagascar.Hinda Deby Itno
 Anafahamika kama mrembo wa Chad, pia anatajwa kuwa mmoja wa wanawake wa marais mwenye bashasha na tabasamu la kipekee, mke wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Chad, Brahim Deby Itno.Zaineb Jammeh Suma
Ni mke wa Rais wa Gambia, Yahaya Jammeh. Zaineb anatajwa kuwa ndiye mwanamke mrembo kuliko wake wengine wa marais katika Afrika. Amezaliwa1977, Rabat nchini Morocco.

Sylvia Bongo Ondimba
Mke wa Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba, Sylvia ndiyo jina alilopewa na wazazi wake mwaka 1965, ni mzaliwa wa Paris Ufaransa, anasifiwa kwa uzuri.