WAWEKEZAJI WA KIGENI WATUPIWE JICHO NA SHUGHULI ZAO

Je ! Huu ndio uwekezaji wenyewe ? Idara ya Uhamiaji mpo wapi ?

ah !  "MGENI WA MUNGU HUYU" mwache ajitafutie riziki ! 

Baadhi ya wawekezaji wa kigeni au pengine watumishi raia wa kigeni wamekuwa
wakivunja sheria za nchi kwa kujiingiza au kufanya shughuli zisizo katika miktaba yao
 ya kazi,au nje ya vibali vyao vya kufanyakazi hapa nchini Tanzania,lakini uvunjwaji wa sheria za nchi unaofanywa na wageni hawa unasaidiwa na sisi wenyewe kwa kuzingatia
zile mila zetu na misemo ya ah !  "MGENI WA MUNGU HUYU" mwache ajitafutie riziki.
Matokeo yake tumekuwa na wachoma mahindi mtaani kutoka china,wabeba zege pia,
Kumradhi pengine makahaba au changudoa kwenye madangulo ya siri.
tunaweza kuwa na wakaanga samaki, walinzi "Kolokoloni" kutoka Thailand na Bangladesh,
inawekana kabisa tunao hapa nchini wapishi na tour guider kutoka nchi za ulaya !
Kwa mtindo na utamaduni wetu huu wa ah! wache "WAGENI WA MUNGU " wajitafutie ridhiki   tutajikuta tunao akina mama ntilie wakigeni.
Tunajiuliza wale wawekezaji wanajiusha na biashara za mitumba au maduka ya nguo kariakoo hivi vibali aliwapa nani? yaani muuza mtumba na duka la sukari atoke china,Yemen,Bangladesh ulaya ! hii kweli inaingia akilini kwa watanzania?
Sasa wawekezaji hawa kigeni wanafanya shughuli hizi mchana wa jua kali tena kweupe
Mkondo wa sheria ya nchi unavunjwa walinzi wa sheria wako wapi?
Wizara zinazohusika amlioni hili au ndio ah! TUWAACHE WAGENI WA MUNGU wajitafutie ridhiki ?  Watanzania ukarimu ni jadi yetu ! misemo hii haifanani kabisa
na ukiwikaji wa sheria za uhamiaji na ajira za nchi, kwani katu kwame uruma na
haki havikai pamoja.