Kanisa lisilo Rasmi Lavunjwa Kawe
Kanisa la lisilo rasmi la mchungaji ngwajima lililokuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe, limeamuriwa kuondoka mara moja na ku
wacha eneo hilo wazi kwa ajili ya maendeleo ya watu wa kawe. Kanisa hilo ambalo kwa muda mrefu lemekuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu na kusababisha usumbufu na kero kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo. Katika Barua iliosainiwa na Meneja wa Mkoa wa kinondoni wa shirika la nyumba la Taifa imesisitiza kwamba pamoja na kutambuliwa umuhimu wa kanisa hilo kuendesha shughuli zake lakini shirika hilo halitaweza kutoa ruhusa kwa kanisa hilo kuendelea kufanya mahubiri katika viwanja hivyo,kwani shirika hilo limeshaanza kutumia Viwanja hivyo kwa maendeleo ya wananchi wa KAWE ikiwa ni ujenzi wa makazi n.k Bw Masika ametoa siku 30 tu ili Mchungaji Ngwajima kujitayarisha na kuwacha viwanja hivyo wazi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
0 Comments