Alexander Zakharchenko, kiongozi wa waasi.
Kiongozi wa cheo cha juu zaidi anayeiunga mkono Urusi katika eneo linalothibitiwa na waasi mashariki mwa Ukrain amesema kuwa usitishwaji wa mapigano ulioafikiwa mapema mwaka huu na serikali hautadumu.
Alexander Zakharchenko aliiambia BBC kuwa maafikiano ya Minsk yangefanikiwa tu ikiwa serikali ya Ukrain ingetambua jamhuri iliyojitenga anayoiongoza eneo la Donetsk.

Bwana Zakharchenko aliongeza kuwa kile angependa kuona ni kupanuka zaidi kwa eneo hilo.
Chini ya makubaliano ya Minsk ambayo yaliungwa mkono na Urusi , Ujerumani na Ufaransa , serikali ya Ukrain ungerejesha mipaka chini ya udhibiti wake.
Mapigano yameendelea licha ya kuwepo kwa makubaliano hayo.