Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi wa CCM, Dk. John Magufuli na Mgombea mwenza Samia Salum leo .
Msafara wa Magufuli ukipita kwenye makutano ya baabara ya Morogoro na Bibi Titi
 Mwananchi akipunga mkono kufuarhia msafara wa Magufuli.
 Wananchi akipunga mkono kufuarhia msafara wa Dk. John Magufuli wakati ukipita kwenye baabara ya Bibi Titi Mohammed, mgombea huyo akienda kuchuua fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 Mgombea mteue wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli akiigia Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi huku akisindikizwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, John Magufuli akisaini fomu maalum, baada ya kuingia Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua fomu za kuomba kugombea urais. Kulia ni Mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan
 Dk. Magufuli akisaini fomu maalum
 Mgombea Mwenza, Samia Suluhu Hassan akitia saini fomu hizo maalum
 Mgombea Mwenza, Samia Suluhu Hassan akitia saini fomu hizo maalum
 Ofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Adam Nyando akimpatia maelezo muhimu, Dk. Magufuli kabla ya kumkabidhi
 Ofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Adam Nyando akimpatia maelezo muhimu, Dk. Magufuli kabla ya kumkabidhi
 Ofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Adam Nyando akimpatia maelezo muhimu, Dk. Magufuli kabla ya kumkabidhi
 Ofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Adam Nyando akimkabidhi Dk. Magufuli mkoba wenye fomu zote za kuomba urais. Huku Mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassani na Katibu wa CCM, Abdlrahman Kinana wakishuhudia kwa makini
 Ofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Adam Nyando akimkabidhi Dk. Magufuli mkoba wenye fomu zote za kuomba urais. Huku Mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassani akishuhudia kwa makini
 Dk. Magufuli na mgombea mwenza wake Samia Suluhu Hassan wakionyesha mkoba wenye fomu zao, nje Ofisi ya Tume
 Maelfu ya wananchi wakimsindikiza Dk. Magufuli kurejea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, baada ya kuchukua fomu
 Maelfu ya wananchi wakimsindikiza Dk. Magufuli kurejea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, baada ya kuchukua fomu
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihamasisha  umati wa wananchi waliokuwa wamefurika kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, wakimsubiri kumpokea Dk. Magufuli akirejea kwenye Ofisi hiyo baada ya kuchukua fomu NEC.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, ili amkaribishe jukwaani, kuonyesha fomu zake, mgobea Mteule wa Urais wa tiketi ya CCM, Dk. John Maguli, kwenye Ofisi ya CCM Lumumba
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na umati wa wananchi kabla ya kumkaribisha Dk. Magufuli kuzungumza na wananchi baada ya kurejea na fomu zake, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 "Fomu ndiyo hizi", Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimsaidia Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli kuonyesha fomu za kuwania Urais kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, alizowasili nazo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam
 Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, akizungumza na wananchi kwenye viwanja vya Ofisi Ndgo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya kurejea na fomu yake ya kuwania Urais
 Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, akizungumza na wananchi kwenye viwanja vya Ofisi Ndgo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya kurejea na fomu yake ya kuwania Urais
 Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, akiserebuka kidogo muziki wa TOT baada ya kuzungumza na umati wa wananchi kwenye viwanja vya Ofisi Ndgo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya kurejea na fomu yake ya kuwania Urais
 Dk. Magufuli akiwashukuru wananchi kwa mapokezi waliyopmpa
 Kisha akawaanga kabla ya Rais Kikwete kuja kumchukua jukwaani
 Rais Kikwete, Naye akajiunga kucheza muziki kidoogo wa TOT kabla ya kuwashusha jukwaani Dk. Magufuli na mgombea mwenza Samia Suluhu Hassani
 Dk. Magufuli akiwaaga wananchi baada ya kumalizika mkutano huo wa mapokezi yake
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwaanga wananchi baada ya mapokezi hayo ya Dk. Magufuli, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba.
 
>HALI ILIVYOKUWA KWENYE OFISI NDOGO YA MAKAO MAKUU YA CCM LUMUMBA KABLA YA DK. MAGUFULI KWENDA KUCHUKUA FOMU
 Kikundi cha Tanzania One Theatre, kikitumbuiza, mbele ya Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini Dar es Salaam, wakati akisubiriwa Dk. Magufuli na mgombea mweza wake kuwasili kwenye Ofisi hiyo kabla ya kwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua fomu leo
 Mjumbe wa Kamati Kuu ambaye pia ni Mkumbe wa NEC, Uchumi na Fedha Mama Zakia Meghji akiongoza baadhi ya wana CCM kuserebuka wimbo wa TOT
 "Sikia Bwana, asikudanganye mtu CCM ndiyo Chama dume..." Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimwambia Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dinas Masaburi, wakati akisubiwa Dk. Magufuli kufika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
"Hapa tumejipanga hadi wapinzani waisome namba" Kinana akimwambia Naibu Katibu Mkuu wake, Rajabu Luhavi wakati akisubiwa Dk. Magufuli kufika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha mgombea mwenza Samia Suhulu Hassan, baada ya kuwasili
 Katibu wa NEC, Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akisalimiana na mgombea Mwenza Samia Suluhu Hassa baada ya kuwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM. Dk. Asha-Rose ni miongoni mwa waomba kuwania Urais kwa tiketi ya CCM ambaye alifanikiwa kuingia tatu bora katika mchakato wa kumpata mgombea wa CCM uliomuibua Dk. Magufuli
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akifurahia jambo na Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa, wakati akisubiwa Dk. Magufuli kufika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Baadhi ya viongozi na wana CCM na Makada wa CCM wakimsubiri Dk. Magufuli
 Msafara wa mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli ukiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Dk. Magufuli akisalimia umati wa wananchi baada ya kuwasili Ofisi ya CCM, Lumumba
 Wananchi wakimpungia mikono Dk. Magufuli baada ya kuwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Katibu wa NEC, Oganaizesheni CCM, Muhammed Seif Khatib akimlaki Mgombea Mteule wa Urais wa CCM, Dk. Magufuli baada ya kuingia chumba cha mapumziko kwa muda, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Dk. Magufuli akimsalimia Dk. Fenela Mkangara baada ya kuwasili chumba cha mapumziko kwa muda katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba
 Dk. Magufuli akimsalimia Dk. Didas Masaburi
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akizungumza na Dk. Magufuli katika chumba cha mapumziko kwa muda
 Dk. Magufuli akiwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM
 Dk. Magufuli akiteta jambo na Dk. Asha-Rose Migiro
 Baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwa katika chumba cha mapumziko ya muda baada ya kuwasili Dk. Magufuli
 Mazungumzo ya hapa na pale yakiendelea
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akizungumza na Dk. Asha-Rose Migiro na Muhammed Seif Khatib
 Dk. Magufuli akifurahia jambo na Mwenyekiti wa UWT, Sohia Simba. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida
 
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiteta jambo na Dk. Magufuli
 Nape akipata ushauri kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara, Philip Mangula
 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akisalimia na Silaa. Kulia ni Dk Hussein Mwinyi
 Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali akimsalimia mgombea mwenza
 Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali akimsalimia Dk. Magufuli
 Dk. Magufui akimsikiliza kwa makini wakati Madabida akimweleza jambo
 Dk. Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Ilala Mussa Zungu
 Dk Asha Rose Migiro akiteta jambo na Sophia Simba na Amina Makilagi
 Dk Magufuli akisalimiana na Abbas Mtemvu
 Dk. Magufuli akitoka chumba cha mapumziko ya muda tayari kwa safari ya kwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi
 Dk. Magufuli akiwasalimia wananchi kabla ya kuanza safari
 Dk. Magufuli akiwasalimia wananchi kabla ya kuanza safari
Mgombea mteule wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli na mgombea mwenza wake wakiwa katika gari la wazi kutoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, kwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Picha zote na Bashir Nkoromo