jokate ali kibaJokate Mwegelo ‘Kidoti’ akiwa na Ali Kiba.
Shani ramadhani
Not true! Staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amekanusha vikali madai kwamba hivi karibuni alitimuliwa nyumbani kwa ‘mtu’ wake, Ali Saleh Kiba maeneo ya Kunduchi-Beach, Dar.

Awali ilisemekana kwamba, mama mzazi wa Kiba ndiye aliyemtimua Jokate kwa kigezo kuwa hamkubali kwani mwanaye ana mchumba mwingine ambaye yupo nje ya nchi.
Kabla ya Jokate kukanusha, gazeti hili lilimuuliza Kiba juu ya ishu hiyo ambapo alifunguka: ““Heee! Hizo taarifa ndiyo nazisikia, hakuna kitu kama hicho halafu mimi na Jokate ni marafiki tu.”
Kwa upande wake Jokate alikuja juu kwamba anazushiwa tu na kwamba hajafukuzwa nyumbani kwa Kiba.
“Sijatimuliwa kwa Kiba huo ni uzushi,” alisema Jokate.