Nshimirimana
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ameomba utulivu baada ya wapiganaji waliovalia magwanda ya kijeshi kumuua mmoja ya majenerali walio na ushawishi mkubwa serikalini.
Katika hotuba kwa taifa muda mchache tu baada ya shambulio hilo,Nkurunziza aliomba utulivu akisema kuwa kisasi kitamaliza kizazi chote.

Hizi ni baadhi ya nukuu za hotuba hiyo.
''Burundi imempoteza mtumishi mkubwa ,jenerali Adolphe Nshimirimana alikuwa alifanya kazi kwa bidii.Natoa wito kwa idara ya usalama kuanzisha uchunguzi ndani ya wiki moja ili wahalifu watambuliwe na kushtakiwa.Nawataka raia wote wa Burundi kuwa watulivu na kuungana.''