Mke wa mwanamuziki wa Nigeria Peter, Lola Omotayo.
Lagos, Nigeria
SEPTEMBA 2, mwaka huu ilikuwa ni siku nzuri ya kusherehekea kuzaliwa kwa mke wa staa wa muziki nchini Naija anayeund la P-Square, Peter, Lola Omotayo ambapo staa huyo alimfagilia balaa.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Peter alishea na mashabiki wake kumtakia heri ya kuzaliwa kwa kuandika maneno matamu.“Maisha yangu bila ya wewe ni sawa na mto pasipo maji. Umefanya maisha yangu yawe mazuri kila muda. Wewe siyo mke wangu tu, bali ni maisha yangu.
Heri ya kuzaliwa mpenzi,” aliandika.Peter na mkewe wana watoto wawili aliozaa na Lola ambao ni Cameron na Aliona.