Image copyrightAP
Image captionGari iliyolipuliwa na Bomu nchini Iraq
Bomu lililotegwa ndani ya gari limelipuka na kuwauwa zaidi ya watu sitini nchini Iraq,katika jimbo la Mashariki la Diyala.bomu hilo lililenga mtaa wa kibishara ambapo zaidi ya watu arobaini walifariki huku pia zaidi ya hamsini kujeruhiwa.
Shambulio jingine lilitokea katika mji wa kusini mwa Basra,ambao kwa mara nyingi haukuwahi kukumbwa na milipuko nchini humo.Maofisa mjini humo wanasema bomu hilo lilitegwa katika mtaa wa al Zubair liliwauwa watu kumi.
Kundi la kiislam la IS limethibitisha kuhusika katika mashambulizi hayo.Katika mji wa Baghdad polisi wamesema kuwa bomu lililotegwa ndani ya gari liliwauwa watu kumi na tatu katika kitongoji cha Husseiniya.