Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amelifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri kufuatia shinikizo ya uma kwamba idadi kubwa ya mawaziri wake ni wafisadi.
Katika baraza la mawaziri lililoongezwa wizara moja,amewaondoa mawaziri sita wanaokabiliwa na kashfa za ufisadi.
Baraza jipya la mawaziri lenye wizara 20 lina mawaziri wanne wanawake.