Ubelgiji imewakamata watu 16 katika operesheni ya polisi kupambana na ugaidi mjini Brussels.
Katika msako huo, nyumba kumi na tisa zimekaguliwa, ingawa hakuna silaha au mabomu yaliyokamatwa.
Ingawa mtuhumiwa mkuu wa shambulio lililotokea mjini Paris, Salah Abdeslam, hajakamatwa.
Operesheni hiyo ya polisi kuhusiana na tishio la ugaidi mjini Brussels imemalizika bila kupatikana kwa vidhibitisho vya kutosha.
Hata hivyo mamlaka ya mji huo imeweza kuongeza muda ili kufanya uchunguzi Zaidi wa tukio hilo katika mji wa Brussels.
Kwa upande wake,Waziri Mkuu wa Ubelgiji , Charles Michel , amesema shule, vyuo vikuu vitafungwa , na usafiri wa treni ya ardhini utasitishwa.