Solange Knowles.
MDOGO wa mwimbaji maarufu wa kike na mwanamitindo wa Marekani, Beyonce Knowles aitwaye Solange Knowles hivi majuzi amepoteza pete yake ya harusi wakati wa hafla moja huko New Orleans nchini Marekani na ametoa bonge la zawadi – kwa kupitia mashabiki wake — kwa mtu ambaye ataiokota na kumpelekea.
Solange anaanimi aliipoteza pete yake katika mitaa ya Toledano na Foucher jijini New York ambapo ametoa tangazo kwa atakayeiokota pete hiyo na kumpa atapata zawadi.
Pete hiyo ilitolewa kwa Solange na mme wake mwenye umri wa miaka 52, Alan Ferguson, siku ya ndoa yao mwaka 2014 Hali halisi inasema kwamba Solange anaogopa kumwambia mumewe kwamba amepoteza pete hiyo kwani si rahisi kwa mumewe kuamini mkewe anaweza kupoteza pete yake kiuzembe namna hiyo.
0 Comments