Taarifa kutoka Sudan Kusini zinasema mamia ya watu, wengi wao wakiwa ni wanajeshi wameuawa katika mapambano baina ya vikosi vyenye uhasama katika mji mkuu wa Juba.
Mwandishi mmoja wa habari aliyeko mjini Juba amesema mapigano yameendelea mpaka mapema saa za asubuh ya Jumamosi.
Wanajeshi wametanda kwenye mitaa huku watu wachache wakionekana kutoka nje.
Daktari mmoja amesema mili mingi imepelekwa hospitali huku chumba cha kuhifadhia maiti kikiwa kimejaa.

Image captionSudan Kusini

Mapigano baina ya wanajeshi watiifu wa Rais Salva Kiiri dhidi ya Makamu wa rais Riek Machar yalianza tangu siku ya Alhamis.
Sudan Kusini inatimiza miaka mitano ya Uhuru na kuanzishwa kwake lakini hakuna sherehe zitakazofanywa.