Hakimu huko nchini Brazil ameruhusu maandamano ya amani ya kisiasa wakati wa michezo ya olimpiki inayoendelea huko mjini Rio.

Uhuru wa kujieleza

Hakimu amesema kuwa kuwaondoa waandamanaji hao ni ukiukwaji wa uhuru wa kujieleza. Amepokea maombi ya kuruhusu maandamano hayo kutoka kwa chombo cha serikali cha kutetea maslahi ya umma, hata hivyo, waandaji wa michezo hiyo wanatarajia kupinga uamuzi huo.