Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akitembelea Kituo kikuu Ubungo cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani, leo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza na sehemu ya Wananchi waliokuwepo kwenye Kituo Kikuu cha Ubungo, Jijini Dar es salaam leo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiwasalimia wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amemtaka Mkurugenzi wa jiji kuanza  mchakato wa kuhamisha kituo kikuu cha mabasi ya mkoani cha ubungo  kuhamia Mbezi mwisho 

Makonda ameyasema hayo leo wakati alipotembelea  kituo hicho leo, amesema kituo hicho kimeelemewa na idadi ya kubwa ya wasafiri huku miundombinu haiendani na utoaji wa huduma kwa wasafiri wanaotumia kituo hicho.

Makonda  amesema kuwa baada ya kituo hicho kuhama panatakiwa kufanyika  uwekezaji wa soko kubwa  ili kupunguza msongamano wa watu katika soko la Kariakoo.

Aidha Makonda amesema kuwa uamuzi huo umetokana na kuonekana kwa kituo hicho kuwa kidogo na kushindwa kutoa huduma ya usafirishaji ya abiria wanaoingia na kutoka katika mikoa mbalimbali.

Makonda ameutaka uongozi wa kituo hicho  kufunga taa maeneo yote kutokana na kutawala kwa giza nyakati za  usiku,ambapo ni  hatari kwa usalama wa abiria  wanaoshuka  nyakati hizo.
RC Makonda pia amepiga marufuku kukamata magari kwa kigezo cha maegesho, wakati hakuna alama zinazoonyesha sehemu ya kuegesha magari.