Mapigano makali yanaendelea mjini Aleppo Syria. Umoja wa mataifa unazungumza na Urusi juu ya kusimamisha mapigano kwa ajili ya utoaji wa misaada kwa watu zaidi ya milioni mbili waliopo katika miji iliyojitenga ya Syria.

Siku ya Jumapili vikosi vya waasi viliharibu huduma muhimu Magharibi mwa Aleppo
Image captionSiku ya Jumapili vikosi vya waasi viliharibu huduma muhimu Magharibi mwa Aleppo

Urusi ilitangaza kusimamisha mapigano dhidi ya waasi kwa masaa matatu kila siku lakini umoja wa mataifa unasema hayatoshi,wanataka masaa 48 ambayo yanatosha kusambaza misaada na kuokoa majeruhi sambamba na wagonjwa.

Zaidi ya wananchi 250,000 wanakosa huduma muhimu mjini Aleppo kutokana na vita
Image captionZaidi ya wananchi 250,000 wanakosa huduma muhimu mjini Aleppo kutokana na vita