Walinda amani tisa wa Muungano wa Afrika wamefungwa jela kwa kushiriki katika bishara ya uuzaji mafuta nchini Somalia.
Wanajeshi hao ambao wote ni kutoka nchini Uganda, wamehukumiwa vifungo vya kati ya mwaka moja na miaka mitatu na mahakama ya kijeshi ya Uganda.

Watatu kati ya wanajeshi hao pia wamefutwa kutoka jeshini.
Hii ndiyo mara ya kwanza mahakama ya kijeshi ya Muungano wa Afrika, imefanya kikao nchini Somalia tangu wanajeshi hao wapelekwe nchini humo miaka tisa iliyopita.
Uganda ndiye mchangiaji mkubwa wa wanajeshi wa kikosi cha wanajeshi 22,000, kinachopigana na wanamgambo nchini Somalia.