Mtandao wa Yahoo umethibitisha kuwa wadukuzi wamedukua taarifa za zaidi ya watumiaji milioni mia tano katika akaunti zake za watumiaji.
Hata hivyo Yahoo imesema inaamini kuwa shambulio la kimtandao la mwaka 2014 lilikuwa limefadhiliwa na serikali.

Data zilizoibwa ni pamoja na majina, anuani za barua pepe, namba za simu, tarehe za kuzaliwa na nywila za watumiaji ama (Password). Lakini wadukuzi hao hawakugusa kadi za malipo na taarifa za akaunti za kibenki.
Watumiaji wa mtandao huo wameshauriwa kubadilisha nywila zao (password) zao ili kuepuka udukuzi wa kimtandao.