Wakati Donald Trump na Hillary Clinton walipokwea jukwaani St Louis kwa mjadala wa pili kati ya mitatu iliyopangwa, hakupeana salamu kwa mikono , jambo lililodhihirisha chuki ambayo ingeendelea katika kipindi kizima cha mjadala huo.
Donald Trump ametangualia kwa kutetea matusi aliyotoa kuhusu kuwagusa wanawake katika sehemu za siri kwa kumshambulia Hillary Clinton na mumewe.
Mgombea huyo wa chama cha Republican, amekana kamwe hajawanyanyasa wanawake kingono, lakini akageuza hasira kwa aliyekuwa rais wa Marekani Bill Clinton katika majibizano makali kwenye mjadala huo
"Hakuna mtu katika historia ya siasa ambaye amewanyanyasa wanawake kiasi hicho," alisema.
Hillary Clinton alikataa kujibu tuhuma hizo dhidi ya mumewe.
Matamshi ya bwana Trump dhidi ya failia ya Clintons yalijiri baada ya muendesha mjadala Anderson Cooper kumuuliza kuhusu kanda ya video ya mwaka 2005 iliyosambazwa katika vyombo vya habari Ijumaa iliyomfichua Trump akijigamba kuhusu kuwagusa wanawake katika sehemu zao za siri.

Hillary Clinton na Donald Trump katika mjadala wa UraisImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionDonald Trump na Hillary Clinton katika mjadala wa Urais

Lakini alipoendelea kuulizwa kuhusu iwapo alimnyanyasa kingono mwanamke yoyote, alikana kufanya hivyo na badala yake akamulika tuhuma zilizomuandamana Bill Clinton katika siku za nyuma.
Hakuna mashtaka ya uhalifu yaliowasilishwa dhidi ya Bwana Clinton katika tuhuma zozote z unyanyasaji wa kingono.
Wagombea hao wawili bila walizozana kuhusu mzozo wa Syria, Uchokozi wa Urusi, na hatua ya bwana Trump kukata kutangaza malipo yake ya kodi na mpango wake wa ukaguzi mkali kwa wahamiaji wanaowasili kutoka mataifa yanayohusishwana ugaidi.
Hatimaye mjadala ulikamilika wakati mwanamume mmoja kutoka umati uliokusanyika kufuatilia mjadala huo, alipowauliza wagombea hao wawili kusema kitu kimoja kizuri kumhusu mwenzake.
Mgombea wa chama cha Democrat Hillary Clinton akasema watoto wake Trump wanamdhihirisha ni mtu wa aina gani.
Naye Trump akamtaja mpinzani wake kuwa "mpiganaji" asiye kata tamaa.