Jana Jumapili Oktoba 09, 2016 kuanzia majira ya saa nane mchana hadi saa 12 jioni kulifanyika Tamasha Kubwa la Kusifu na Kuabudu, katika Kanisa la Kimataifa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza.

Mamia ya watu/waumini walijitokeza kwa wingi katika tamasha hilo ambalo hakika lilifanya na kugusa nyoyo za wengi.


Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani) alielezea kufurahishwa na tamasha hilo na namna lilivyofana huku akisisitiza wanadamu kuwa na desturi ya Kusifu na Kumuabudu Mungu kwani kupitia ibada hiyo, milango ya mbinguni hufunguka.
Na BMG
Kushoto ni mwimbaji wa nyimbo za injili hususani za kusifu na kuabudu, Yusuph Nghumba, akiimba katika tamasha hilo. Kulia ni mkewe. 

Licha ya kwamba mwimbaji huyo anakabiriwa na tatizo la kutoona lililomkumba ghafla ukubwani, lakini bado anamsifu na kumuabudu Mungu katika roho na kweli na anaendelea kubarikiwa licha ya jaribu hilo la kimwili kwani ipo siku atauona ukuu wa Mungu.
Wa pili kushoto ni mwimbaji wa nyimbo za injili hususani za kusifu na kuabudu, Yusuph Nghumba, akiimba katika tamasha hilo. Wa pili kulia ni mkewe na wa kwanza kushoto ni mmoja wa watoto wao. Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Vijana kanisa la EAGT Lumala Mpya ambaye pia ni mwimbaji mahiri wa kusifu na kuabudu.

Licha ya kwamba mwimbaji huyo anakabiriwa na tatizo la kutoona lililomkumba ghafla ukubwani, lakini bado anamsifu na kumuabudu Mungu katika roho na kweli na anaendelea kubarikiwa licha ya jaribu hilo la kimwili kwani ipo siku atauona ukuu wa Mungu.
Praise and Worship Team kutoka Kanisa jirani la CAG Sabasaba Jijini Mwanza, wakihudumu kwenye tamasha hilo.
Praise and Worship Team kutoka Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Sabasaba Jijini Mwanza, waliokuwa wenyeji wa tamasha la Kusifu na Kuabudu, wakihudumu.
Mamia ya waliohudhuria tamasha hilo, wakimsifu Mungu 
Praise and Worship Team kutoka Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Sabasaba Jijini Mwanza, waliokuwa wenyeji wa tamasha la Kusifu na Kuabudu, wakihudumu.
Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola (mwenye suti) akiungana na waumini wengine kumsifu Mungu kwa roho na kweli.
Mmoja wa waimbaji mahiri kutoka Kanisa la EAGT Lumala Mpya akihudumu kwenye tamasha la Kusifu na kuabudu lililofanyika jana kwenye kanisa hilo.
Mwenyekiti wa Vijana kanisa la EAGT Lumala Mpya ambaye pia ni mmoja wa waimbaji mahiri wa kusifu na kuabudu akihudumu kwenye tamasha hilo.
Wote wanaomsifu na kumuabudu Mungu kwa roho na kweli, hubarikiwa
Hakika Tamasha la Kusifu na Kuabudu lilifanya sana ndani ya Kanisa la Kimataifa la EAGT Lumala Mpya hivyo usikose tamasha lijalo ambalo utajuzwa pia kupitia mtandao huu.
Bonyeza HAPA Kwa Taarifa Zaidi.