Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  amekutana na kuzungumza na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa nyumbani kwake mjini Dodoma akiwa njiani kuelekea mkoani Iringa kuzindua kikosi kazi cha Taifa cha bonde la mto Ruaha Mkuu.