Korea ya Kaskazini imesitisha mazungumzo yaliyotarajiwa kufanyika mapema wiki hii dhidi ya Korea ya Kusini kwa sababu ya kuchukizwa kwake na mazoezi ya kijeshi ya pamoja na Marekani.

Maafisa wa shirika la habari la Korea ya Kaskazini KCNA wameeleza kuwa mazoezi hayo ni sehemu ya mazoezi ya "chuki" na kuyachukulia kama mazoezi ya uvamizi.Lakini pia kuna onyo lililotolewa na Marekani juu ya hatima ya mkutano wa kihistoria kati ya Kim Jong-un na Rais wa Marekani Donald Trump ambao umepangwa tarehe 12 Juni.
Ikumbukwe kwamba katika ya mwezi wa tatu mwaka huu , Mr Trump aliushangaza ulimwengu kwa kukubali mwaliko wa kukutana na rasi Kim, na kujinasibu kuwa "Tutajaribu kuufanya mkutano wetu kuwa wa wakati wa pekee wa Amani ya Dunia!" raisi wa Marekani aliandika haya kwenye mtandao wa tweeter wakati huo kama ilivyo kawaida yake.
Idara ya Serikali ya Marekani inasema ilikuwa inaendelea kujiandaa kwa mkutano baina ya viongozi hao wawili Trump na Kim nchini Singapore na kwamba hakukuwa na taarifa zozote za kuahirishwa kwa mkutano huo kulingana na nafasi ya Korea ya Kaskazini.
Huu ni kama mchezo wa bahati nasibu wa siasa za karne ya ishirini na moja
North Korea and South KoreaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionNdege za kivita zikiwa tayari kwa matumizi
Tuangalie namna kiongozi wa Korea ya Kaskazini alivyoweza kusafiri, akiambatana na ndege mia moja za kivita, ikiwa ni pamoja na idadi isiyojulikana ya makombora aina ya B-52 na ndege ndogo aina ya F-15K.
Korea na Amerika ya Kusini daima zimesisitiza kuwa kekee hizo ni kwa madhumuni ya ulinzi,ingawa ni kinyume na makubaliano ya utetezi wa pamoja walio tiliana saini mwaka 1953 , ingawa imejitetea kwamba mazoezi ni muhimu ili kuimarisha utayari wao ikiwa kuna mashambulizi ya nje.
Mkutano huo ulipaswa kufanyika eneo la Panmunjom, kwenye eneo la kiwanja cha kijeshi katika ukanda wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili.
Wawakilishi kutoka pande zote walikubaliana kujadiliana hatua za kufuatilia juu ya mikataba waliyoifanya katika mkutano wa nadra tarehe 27 Aprili.
Kim Jong-un wa Korea ya Kaskazini na Mwenza wake Jae wa Korea Kusini wamekubaliana kufanya kazi ya kuondoa uhalifu wa silaha za nyuklia katika rasi zao baada ya mazungumzo hayo.