Kwa jinsi wananchi wanavyopenda nyimbo za msanii Fid Q maarufu kama Ngosha  waling'ang'ania asitoke uwanjani na aendelee kuwaimbia wapate burudani zaidi ila Askali waliingilia kati na kumuondosha huku wakimlinda kama mfalme.
 Kama unaujua wimbo wa IVETA basi huyu ndiye muimbaji wa nyimbo hiyo,anakwenda kwa jina la Sajna hapo anakonga nyoyo za watu mkoani Shinyanga.
Bidada Mwasiti ambaye hakubaki nyuma kuwapa watu burudani kwa sauti yake nyororo,kila mmoja alipata  burudani uwanjani hapo. 
 Kama unavyojionea mtiti(umati)wa watu waliokuwa uwanjani hapo wakijipatia burudani toka kwa wasanii mbalimbali wa Bongofleva.
Kutoka kushoto ni Chege na kulia ni Muheshimiwa Temba kutoka kundi la TMK hawa nao walishangiliwa kila walipopanda jukwaani kiasi kwamba waliomba kupanda tena na tena.Fiesta ilifana vilivyo mkoani hapo.(picha na G sengo)