Bwana Habib baada ya kutoka tu ukumbini yeye na mke wake bi Monica walikwenda moja kwa moja Hotel ya Appolo iliyopo mjini Almere kwa mapumziko ya wiki moja kabla ya kurejea kwenye ujenzi wa Taifa.pichani bi Monica akiangalia harusi yake kwa njia ya mtandao kupitia blog ya Maganga One.
Wakijiangalia jinsi walivyopendeza kwa njia ya mtandao toka Maganga One Blog,Hongereni sana maharusi Maganga One inawatakia mapumziko mazuri hotelini hapo.Bwana Habib kwa niaba ya mkewe wametoa shukrani za dhati kwa kila mmoja aliyeweza kufanikisha shughuli nzima ya harusi yao na kwamba kwa kila mwenye kumuhitaji kwa kipindi hiki simu yake ipo on muda wote.