![]() |
Maandamano Misri |
Mahakama kuu ya katiba nchini Misri imesababisha hali ya wasiwasi nchini humo baada ya kutangaza kuwa uchaguzi wa wabunge uliofanyika mwaka jana ulikuwa kinyume cha katiba na kutaka ufanyike upya.
Uamuzi huo wa mahakama uliotolewa siku mbili kabla ya kufanyika duru ya pili ya kinyang'anyiro cha urais, unalipa baraza la utawala wa kijeshi nguvu za bunge. Kulingana na wachambuzi wa masuala ya kisiasa, uamuzi huo una athari kubwa hasa kwa kuwa umetolewa kabla ya kufanyika kwa duru ya pili ya uchaguzi mwishoni mwa juma, na inamaanisha sasa kwamba mamlaka ya bunge nchini humo yamo chini ya baraza kuu la Kijeshi ambalo lilipewa jukumu la kuongoza Misri katika kipindi cha mpito baada ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Hosni Mubarak kung'olewa madarakani.
0 Comments