Waziri wa Nchi, Uhusiano na Uratibu, Mhe. Stephen Wassira (Kulia) akimsikiliza kwa makini Mhe. Fan Xiaojian, Waziri, Ofisi Kiongozi ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, inayohusika na masuala ya Maendeleo na Kupunguza Umaskini (Katikati). Kushoto ni Mkalimani wa Waziri huyo.
Naibu Katibu Mtendaji (Uzalishaji) wa Tume ya Mipango, Maduka Kessy (Katikati) akizungumza na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango (Kushoto) akizungumza na mmoja wa washiriki wa Kongamano hilo Li Xin kutoka China.
Wadau wa habari nao hawakuwa nyuma katika kunasa matukio ya Kongamano hilo.
Washiriki wa Kongamano wakiwa makini kufuatilia mawasilisho na mada mbali mbali zilizokuwa zikitolewa.