Watu 54 wamefariki dunia wakati wakijaribu kuvuka bahari kutoka
Libya kwenda Italia kwa kutumia boti la mpira wa kujaza pumzi, kwa mujibu wa
shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi.
Mtu pekee aliyenusurika balaa hilo, aliyeokotwa na wavuvi kutoka
Tunisia,amesema kuwa wenzake walizama kutokana na kiu baada ya kusafiri kwa
zaidi ya siku kumi na tano baharini.
Ameliambia shirika la UNHCR kuwa walikaribia pwania ya Italia lakini
wakasumbuliwa na mawimbi makali yaliyowasukuma hadi boti lao lilipoishiwa na
pumzi.
Inasadikiwa kuwa wengi wa watu hao ni kutoka Eritrea.
Manusura ambaye ni raia wa Eritrea pia, aliokolewa na wavuvi wa Tunisia nje
ya pwani ya Tunisia na kwa wakati huu anatunzwa kwenye hospitali ya nchini
Tunisia.
Aliliambia shirika la UNHCR kuwa kundi la watu 55 liliondoka Libya mwishoni
mwa mwezi Juni.
Manusura huyu aliendelea kumfahamisha msemaji wa Umoja wa Mataifa Laura
Boldrini kuwa "matatizo yalianza punde baada ya kuvua nanga, na kwa bahati mbaya
hatukuruhusiwa kuchukua hata chupa moja ya maji ya kunywa, kwa hiyo tulipokosa
njia na mwendo wetu kuendelea watu wakaanza kujihisa wagonjwa na kufariki
kutokana na kukosa maji.
According to the UNHCR, around 170 people have died this year trying to reach
Europe from Libya.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya wakimbizi,UNHCR
limesema kuwa hadi watu 1,300 wamefanikiwa kuvuka hadi Italia kupitia bahari
tangu kuanza kwa mwaka huu 2012.
Raia wengi wa Eritrea hujaribu kila njia ili kufika sehemu yoyote ya Ulaya au
Israil kutafuta maisha bora.
Wakosoaji wanasema wanaikimbia serikali dhalimu inayowakandamiza, umasikini
na kulazimishwa kujiunga na Jeshi la Taifa wanapotimizia umri wa miaka
40.
0 Comments