Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi, jana  Ijumaa aliungana na  Mabalozi wengine katika kutia saini kitabu cha Maombolezo  kufuatia kifo cha Rais wa Venezuela,  Hugo Chaves, aliyefariki siku  ya jumanne wiki hii kwa ugonjwa wa  kansa. Kitabu hicho  kilifunguliwa katika Ubalozi wa Kudumu wa  Venezuela katika Umoja wa Mataifa.