KATIKA kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, mwigizaji nyota
nchini Jenifer Kyaka 'Odama' amewataka wanawake kuamka na kufanya kazi
kwa bidii ili kuweza kuondoa utegemezi katika jamii.
Akizungumza na Mwananchi jana Odama ambaye kwa
sasa ni msanii wa kwanza wa kike nchini kumiliki kampuni ya utengenezaji
filamu ya J-Film 4 Life alisema kujiamini pekee ndiko kunakomfanya
mwanamke yoyote kufikia malengo aliyojiwekea katika maisha.
"Kesho (leo) ni siku ya wanawake duniani, lakini
tujiulize ni nini tunakifanya katika kuhakikisha tunasonga mbele? Au
kila siku tutaogopa kufanya jambo tukitegemea wanaume pekee ndio wenye
uwezo?
Tunapaswa kujituma kwa bidii katika kuhakikisha tunatimiza malengo yetu tuliyojiwekea katika maisha,"anasema Odama.
Anasema mwanamke ni kila kitu "kila mtu amezaliwa
na mwanamke, huyu ni mtu wa muhimu katika jamii. Bila kujiheshimu na
kufanya kazi kwa bidii utu wetu hauwezi kutambuliwa, tunapaswa kuwa na
ubunifu."
Ametoa wito kwa kila mwakamke kwa nafasi yake na kwa kazi yake anayoifanya kuongeza bidii zaidi.
Aidha anasema wasanii wengi wa kike wamekuwa
wakihofia kujituma na kufanya kazi ambazo wanaume wanazifanya jambo
linalochangia kuwarudisha nyuma huku tatizo hilo likisababisha uchache
wao katika fani hiyo.
0 Comments