Uchapisha wa Hati za Kusafiria (Pasipoti), nchini umesimama kwa muda baada ya mashine zinazotumika kuharibika anchi limebaini.Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili na baadaye kuthibitishwa na Idara ya Uhamiaji, umeonyesha kuwa tatizo hilo lilianza Januari na litlea hadi Mei mwaka huu.

Kusitishwa kwa huduma hiyo kumesababisha mrundikano wa maombi ya hati hizo, huku waombaji wakWaombaji wanaopigwa kalenda kupata hati hizo ni pamoja na wanaoomba kwa mara ya kwanza na wale wanaotaka mpya baada ya za awali kujaa au kumalizika muda wake.

Kabla ya mashine hiyo kuharibika muombaji aliweza kupata pasipoti yake ndani ya siku saba, baada ya kukamilisha taratibu za uombaji, lakini kutokana na tatizo hilo, imetimia miezi mitatu sasa, waombaji hawajui watapata lini hati hizo.

Baadhi ya waombaji walioongea na gezeti hili walilalamikia kitendo hicho wakisema kinawasababishia usumbufu na kuwakwamisha katika kufanya.Uchunguzi wa gazeti hili unaonyesha kuwa baadhi ya wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji na vishoka, tayari wameanza kujinufaisha na tatizo hilo kwa kuomba rushwa kutoka kwa waombaji hati hizo ili wawatekelezee matakwa yao kwa haraka.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Mbarak Abduwakil alikataa kuzungumzia suala hilo, akidai kuwa amebanwa na vikao ofisini kwake.Hata hivyo, Kaimu Ofisa Uhusiano wa Uhamiaji, Tatu Burhan alikiri kuwepo kwa tatizo hilo, lakini akasema halitokani na mashine zao kuharibika.


“Tatizo hili limetokana na ukosefu wa malighafi toka nje ya nchi. Unajua malighafi hizo tunaziagiza, lakini kwa bahati mbaya hazikuweza kupatikana kwa wakati,” alisema Tatu.


Pamoja na uhaba wa mali ghafi, alisema kwa bado Uhamiaji iliendelea kutoa pasipoti kwa wenye maombi maalumu ya dharura.Alikiri pia kwamba kwa waombaji wasio na dharura maombi yao yaliwekwa kando yakisubiri kuwasili kwa malighafi.


Hata hivyo Tatu alisema kuwa mali ghafi hizo zimeshawasili Bandari ya Dar es Salaam jana na walikuwa katika harakati za kuzitoa.


“Hivi ninavyozungumza (jana) malighafi ghafi hizo tayari zimefika bandarani na tupo kwenye harakati za kuzichukua,” alisema.
                                Alisema kuwa pamoja na malighafi hizo kuwasili ni vigumu kuchapisha pasipoti zote kwa wakati mmoja kutokana na wingi wa maombi.Hata hivyo alisisitiza kuwa Uhamiaji itahakikisha inakamilisha mahitaji ya waombaji wote waliotangulia ili iweza kurejesha utaratibu wa awali kupata pasipoti ndani ya siku saba.

Alisema kuwa waombaji wote waliocheleweshewa hati hizo watakuwa wamepata pasipoti zao ifikapo Aprili mwaka huu kwa kuwa mwishoni mwa mwezi huo, watakuwa wamerejesha utaratibu wa awali wa kupata hati hizo ndani ya siku saba.